Jul 2, 2016

JESHI LA POLISI, WANANCHI WAJIKITA RASMI KATIKA MAPAMBANO NA WAHALIFU

Mkuu wa Polisi wilaya ya Arusha (SSP) Emmanuel Tille akiongea na viongozi wa kata ya Moivaro tarafa ya Suye pamoja na askari wa vikundi vya ulinzi shirikishi wakati wa uzinduzi wa vikundi vinne vya kata hiyo.

Diwani wa kata ya Moivaro Rick Moiro akiongea na askari wa vikundi vya ulinzi shirikishi toka kwenye baadhi ya mitaa ya kata yake mara baada ya uzinduzi wa vikundi hivyo. Mkuu wa Polisi wilaya ya Arusha (SSP) Emmanuel Tille akiwakagua askari wa vikundi vya ulinzi shirikishi kutoka mitaa ya Ngurumausi, Oldonyommasi, Moivaro Kati na Shangarao. Baadhi ya viongozi wa kata ya Moivaro pamoja na askari wa vikundi vipya vya ulinzi shirikishi wakimsikiliza kwa umakini Mkuu wa Polisi wilaya ya Arusha (SSP) Emmanuel Tille hayupo pichani. Mmoja wa wahitimu wa askari wa ulinzi shirikishi katika kata ya Moivaro akikabidhiwa kitambulisho cha kazi kutoka kwa Mkuu wa Polisi wilaya ya Arusha (SSP) Emmanuel Tille.