Naibu
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe Annastazia James
Wambura akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Finland Tanzania Pekka
Hukka wakati wa kukabidhi Bendera ya Taifa kwa timu ya mpira wa miguu
ya wasichana ya Fc Vito Malaika inayoenda kushiriki mashindano ya
Helsinki Cup nchini Finland Julai 8 mwaka huu. ( Picha zote na Raymond
Mushumbusi WHUSM)
Naibu
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe Annastazia James
Wambura (wa pili kulia) akikabidhi Bendera ya Taifa kwa nahodha timu ya
mpira wa miguu Fc Vito Malaika Alia Fikiri (kushoto) kwenda kushiriki
mashindano ya Helsinki Cup nchini Finland Julai 8 mwaka huu.
Naibu
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James
Wambura akizungumza na timu ya mpira wa miguu ya wasichana ya umri wa
miaka 11 Fc Vito Malaika na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika
hafla ya kukabidhi Bendera ya Taifa kwa timu hiyo kwenda kushiriki
mashindano ya mpira wa miguu ya Helsinki Cup nchini Finland Julai 8
mwaka huu kushoto Mwakilishi wa Sport Development Aid Bw. Chigogolo
Mohamed.
Na Raymond Mushumbusi WHUSM
Serikali imeazimia kujenga na kuendeleza shule za michezo zilizopo katika mikoa yote nchini kwa kipindi hiki cha Serikali awamu ya tano.
Azimio hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura wakati akizungumza na timu ya mpira ya miguu ya wasichana ya Fc Vito Malaika katika hafla ya kukabidhi Bendera ya Taifa kwa timu hiyo kwenda kushiriki mashindano ya mpira wa miguu ya Helsinki Cup yatakayofanyika nchini Finland Julai 8 mwaka huu.
“Azima ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuendeleza michezo nchini kwa kuibua vipaji vya michezo na kuviendeleza kuanzia wakiwa shule” Alisema Mhe. Annastazia.
Na Raymond Mushumbusi WHUSM
Serikali imeazimia kujenga na kuendeleza shule za michezo zilizopo katika mikoa yote nchini kwa kipindi hiki cha Serikali awamu ya tano.
Azimio hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura wakati akizungumza na timu ya mpira ya miguu ya wasichana ya Fc Vito Malaika katika hafla ya kukabidhi Bendera ya Taifa kwa timu hiyo kwenda kushiriki mashindano ya mpira wa miguu ya Helsinki Cup yatakayofanyika nchini Finland Julai 8 mwaka huu.
“Azima ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuendeleza michezo nchini kwa kuibua vipaji vya michezo na kuviendeleza kuanzia wakiwa shule” Alisema Mhe. Annastazia.