
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati)
akizungumza na wawekezaji wa Makampuni ya utafiti na uchimbaji wa Mafuta na
Gesi (hawaonekani pichani). Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Utafiti wa Shirika
la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Kelvin Komba, wa pili kulia ni
Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania TPDC, Dkt. James Mataragio na kushoto ni Afisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini,
Mhandisi Albert Diliwa.

Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC),
Dkt. James Mataragio (katikati) akiongea
jambo wakati wa kikao cha Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo
(wa kwanza kushoto) na wawekezaji wa Kampuni za kutatifi na kuchimba mafuta na
gesi nchini. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Utafiti wa Shirika la Maendeleo
ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio.


Baadhi ya Wawekezaji wa Kampuni za kutafiti na kuchimba mafuta na gesi
nchini, wakimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo
(hayupo pichani) wakati wa kikao chake na wawekezaji hao.

Mmoja wa wawakilishi wa Kampuni ya Swala Tanzania, akiwasilisha taarifa
ya mipango ya utekelezaji wa kampuni hiyo wakati wa kikao kati ya Waziri wa Nishati
na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na kampuni hiyo.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Dodsal, K. Surendran, akitoa taarifa ya
utafiti kuhusu Kampuni hiyo kugundua gesi eneo la Ruvu. Wengine wanaomsikiliza
ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati). Mkurugenzi
wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio (wa
pili kulia), Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Utafiti wa TPDC, Kelvin Komba, na
kushoto ni Afisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Albert Diliwa.