Feb 25, 2016

DK KALEMANI AKATAA UTAFITI WA GGM KUHUSU MIPASUKO Ø Aagiza GST kufanya utafiti huo.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (Meza Kuu-mwenye miwani), akiwa kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lulembelwa, Kata ya Lulembelwa, Wilaya ya Mbogwe, Mkoani Geita. Dk Kalemani alisikiliza kero za wananchi hao kuhusu sekta za nishati na madini na aliwajulisha mipango mbalimbali ya Serikali kuhusu masuala ya upatikanaji wa umeme wa uhakika vijijini.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani akisaini Kitabu cha Wageni, ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Manguchie (katikati), kabla ya kuanza ziara yake wilayani humo kushughulikia kero mbalimbali za wananchi kuhusu masuala ya madini.
Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Geita, Fabian Mshai, akisoma taarifa ya kazi ya Ofisi yake kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani), wakati wa ziara yake wilayani humo. Wengine pichani ni viongozi mbalimbali wa Serikali wa Wilaya, Kata na Vijiji pamoja na Maofisa wa Wizara.
Makamu Rais wa GGM anayeshughulikia Mahusiano na Maendeleo ya Jamii, Simon Shayo, akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani) kuhusu msimamo wa Mgodi kuhusiana na malalamiko ya wananchi kuathiriwa nyumba zao kutokana na milipuko inayofanywa na Mgodi huo.
Mbunge wa Jimbo la Geita, Constantine Kanyasu, akizungumza na wananchi wa Geita wakati Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (mwenye miwani) alipofanya ziara ya kazi wilayani humo kutatua kero mbalimbali za wananchi kuhusu masuala ya madini.
Mkazi wa Kijiji cha Katoma wilayani Geita, Malekela Emmanuel akitoa malalamiko yake kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani) kuhusu nyumba yake kuathiriwa na milipuko inayofanywa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM).