Naibu Waziri wa
Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (Meza Kuu-mwenye miwani), akiwa kwenye
mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Lulembelwa, Kata ya Lulembelwa, Wilaya ya
Mbogwe, Mkoani Geita. Dk Kalemani alisikiliza kero za wananchi hao kuhusu sekta
za nishati na madini na aliwajulisha mipango mbalimbali ya Serikali kuhusu
masuala ya upatikanaji wa umeme wa uhakika vijijini.
Naibu Waziri wa
Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani akisaini Kitabu cha Wageni, ofisini kwa
Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Manguchie (katikati), kabla ya kuanza ziara
yake wilayani humo kushughulikia kero mbalimbali za wananchi kuhusu masuala ya
madini.
Kaimu Afisa Madini
Mkazi wa Geita, Fabian Mshai, akisoma taarifa ya kazi ya Ofisi yake kwa Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani), wakati wa
ziara yake wilayani humo. Wengine pichani ni viongozi mbalimbali wa Serikali wa
Wilaya, Kata na Vijiji pamoja na Maofisa wa Wizara.
Makamu Rais wa GGM
anayeshughulikia Mahusiano na Maendeleo ya Jamii, Simon Shayo, akitoa taarifa
kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani)
kuhusu msimamo wa Mgodi kuhusiana na malalamiko ya wananchi kuathiriwa nyumba
zao kutokana na milipuko inayofanywa na Mgodi huo.
Mbunge wa Jimbo la
Geita, Constantine Kanyasu, akizungumza na wananchi wa Geita wakati Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (mwenye miwani) alipofanya
ziara ya kazi wilayani humo kutatua kero mbalimbali za wananchi kuhusu masuala
ya madini.
Mkazi wa Kijiji cha
Katoma wilayani Geita, Malekela Emmanuel akitoa malalamiko yake kwa Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani) kuhusu nyumba
yake kuathiriwa na milipuko inayofanywa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM).