
Afisa
utalii wa hifadhi Taifa Arusha National Park (ANAPA) Samweli Sakinoi
akiwa anawapa maelekezo baadhi ya waandishi waliotembelea hifadhi hiyo

Baadhi ya waandishi waliotembelea hifadhi ya ANAPA.
Na Woinde Shizza,Arusha
Hifadhi
ya taifa Arusha (ANAPA) inakabiliwa na changamoto ya mbalimbali ikiwemo
ya kuzibwa kwa mapito ya wanyama (ushoroba )vilivyo tokana na shughuli
za binadamu kafika vijiji zaidi ya 84 vilivyozunguka hifadhi hiyo.
Akizungumza
na waandishi wa habari afisa utalii wa hifadhi hiyo Samweli Sakinoi
alisema kuwa kufungwa kwa vishoroba hiyo vimesababisha wanyama wengi
kutoingia na kutoka ndani ya hifadhi hiyo jambo ambalo linasababisha
baadhi ya wanyama kutoweka na kusabisha kupungua kwa baadhi ya vivutio
Alisema
kuwa pamoja na hifadhi hiyo kuwa na vivutio mbalimbali ikiwemo uwepo wa
mnyama aina ya mbega mweupe ambaye ni marachache kupatikana katika
hifadhi zingine hapa nchini ,kupanda mlima meru ,utalii wa kutumia
farasi ,utalii wa kumia magari ,pamoja na uwepo wa maziwa mengi madogo
madogo pamoja na utalii wa kupiga makasi kitua ambacho kimefanya utalii
kuongezeko la watalii kuongezeka kutoka watalii 20 hadi 40 wanaoingia
kwa siku.
Ili
kukabiliana na changamoto hiyo mamlaka iyo imeanza utaratibu wa kukutana
na uwongozi wa mkoa wilaya kwa lengo la kuwapatia elimu wananchi
kuepuka kuvamia maeneo ya ifadhi kufanya makazi ,shughulli za kilimo na
ufugaji jambo ambalo lina fukuza wanyama waliozoeya kuishi mazingira ya
asili .
“shughuli
za kibinadamu zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa kutoweka kwa
baadhi ya wanyama hali ambayo inaweza kusababisha kupotea kwa wanyama
katika hifadhi hiyo”alisema Saikononi
Aidha
alisema kuwa kwa sasa ivi wameboresha vivutio vyao na wameongeza
vivutio ambavyo vinaweza kusaidia kuongeza watalii ambapo alibainisha
kuwa kwa sasa ivi wameleta utalii mpya ambao aupo katika hifadhi
zingine ambao ni utalii wa kutumia farasi ambao utalii huu ni mzuri
ambao utalii huu ni mzuri kwani unasaidia wageni wengi kuweza kuona
wanya kiuraisi
Mmoja
wa wananchi wanaishi pembezoni mwa hifadhi hiyo Elituliza Elisa alisema
kuwa amekuwa akinufaika na hifadhi hiyo kwa kukopeshwa fedha kwa riba
nafuu pia pamoja na hafadhi hiyo kuwajengea shule watoto wao.
Aidha
waliitaka hifadhi hiyo iendelee kutoa misaa kwa wananchi ambao
wamezunguka hifadhi hiyo kwa lengo la kunufaika na wageni ambao
waliokuwa wanafanya utalii wa ndani katika hifadhi hiyo.