Feb 25, 2016

kuzibwa kwa ushoroba kunachangia kupotea kwa wanyama hifadhi ya arusha

 Afisa utalii wa hifadhi Taifa  Arusha National Park (ANAPA)  Samweli Sakinoi akiwa anawapa maelekezo baadhi ya waandishi waliotembelea hifadhi hiyo
Baadhi ya waandishi waliotembelea hifadhi ya ANAPA.

Na Woinde Shizza,Arusha
Hifadhi ya taifa Arusha (ANAPA) inakabiliwa na changamoto ya mbalimbali ikiwemo ya kuzibwa kwa mapito ya wanyama (ushoroba )vilivyo tokana na shughuli za binadamu kafika vijiji zaidi ya 84 vilivyozunguka hifadhi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari afisa utalii wa hifadhi hiyo Samweli Sakinoi alisema kuwa kufungwa kwa vishoroba hiyo vimesababisha wanyama wengi kutoingia na kutoka ndani ya hifadhi hiyo jambo ambalo linasababisha baadhi ya wanyama kutoweka na kusabisha kupungua kwa baadhi ya vivutio
Alisema kuwa pamoja na hifadhi hiyo kuwa na vivutio mbalimbali ikiwemo uwepo wa mnyama aina ya mbega mweupe ambaye ni marachache kupatikana katika hifadhi zingine hapa nchini ,kupanda mlima meru ,utalii wa kutumia farasi ,utalii wa kumia magari ,pamoja na uwepo wa maziwa mengi madogo madogo pamoja na utalii wa kupiga makasi kitua ambacho kimefanya utalii kuongezeko la watalii kuongezeka kutoka watalii 20 hadi 40 wanaoingia kwa siku.
Ili kukabiliana na changamoto hiyo mamlaka iyo imeanza utaratibu wa kukutana na uwongozi wa mkoa wilaya kwa lengo la kuwapatia elimu wananchi kuepuka kuvamia maeneo ya ifadhi kufanya makazi ,shughulli za kilimo na ufugaji jambo ambalo lina fukuza wanyama waliozoeya kuishi mazingira ya asili .

“shughuli za kibinadamu zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa kutoweka  kwa baadhi ya wanyama hali ambayo inaweza kusababisha kupotea kwa wanyama katika hifadhi hiyo”alisema Saikononi
Aidha alisema kuwa kwa sasa  ivi wameboresha vivutio vyao na wameongeza vivutio ambavyo vinaweza kusaidia kuongeza watalii ambapo alibainisha kuwa kwa sasa ivi  wameleta utalii mpya ambao aupo katika hifadhi zingine ambao ni utalii wa kutumia farasi ambao utalii huu ni mzuri ambao utalii huu ni mzuri kwani unasaidia wageni wengi kuweza kuona wanya kiuraisi
Mmoja wa wananchi wanaishi pembezoni mwa hifadhi hiyo Elituliza Elisa alisema kuwa amekuwa  akinufaika na hifadhi hiyo kwa kukopeshwa fedha kwa riba nafuu pia pamoja na hafadhi hiyo kuwajengea shule watoto wao.
Aidha waliitaka hifadhi hiyo iendelee kutoa misaa kwa wananchi ambao wamezunguka hifadhi hiyo kwa lengo la kunufaika na wageni ambao waliokuwa wanafanya utalii wa ndani katika hifadhi hiyo.