Jan 26, 2016

TASAF YATATHMINI SHUGHULI ZAMPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI-PSSN

 Baadhi ya watumishi wa TASAF na Wadau wa Maendeleo wakiwa katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ikiwa ni sehemu ya mapitio ya utekelezaji wa nusu mwaka .
 Baadhi ya watumishi wa TASAF  na Wadau wa Maendeleo wakiwa katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa Mpango wa unusuru Kaya maskini 
 Mmoja wa wadau wa maendeleo (aliyeshika kipaza sauti) akichangia mjadala wa tathmini ya utekelezaji wa hughuli za Mpango wa kunusuru kaya maskini unaotekelezwa na TASAF.
 Baadhiyawatumishiwa TASAF  na wadau wa Maendeleo wakifuatilia maelezo ya tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru  kaya maskini baada ya ziara ya maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya tathmini ya Mpango huo inayofanyika makao makuu ya TASAF.
MkurugenziMtendajiwa TASAF ,Bwana  Ladislaus Mwamanga (kushoto) akijadiliana jambo na Kiongozi wa Benki ya Dunia nchini anayesimamia shughuliza TASAF,Bw. Abdulah Mohamed Muderis (kulia) katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kwenye ukumbi wa mikutano makao makuu ya TASAF-jijini Dar es salaam.

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo unaendelea na kikao cha kutathmini utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kinachofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Mfuko huo jijini Dar es salaam.
Mkutano huo unafuatia ziara zilizofanywa na wadau hao wa maendeleo na maafisa  wa TASAF katika mikoa ya DODOMA,MANYARA,SINGIDA,RUKWA na ZANZIBAR kuona utekelezaji wa Mpango huo uliofanikiwa kuzifikia Zaidi ya kaya Milioni Moja na Laki Moja nchini kote .
Kaya hizo zimenufaika na ruzuku inayotolewa na TASAF kupitia Mpango wa kunusuru kaya Maskini.Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji Bwana Ladislaus Mwamanga amesema utaratibu wa kufanya tathmini ya Mpango huo kwa kutembelea maeneo ya walengwa husaidia kwa kiwango kikubwa kuona picha halisi ya mafanikio n ahata changamoto zinazojitokeza ili kuboresha Zaidi huduma kwa walengwa.
Taarifa kutoka maeneo yaliyotemebelewa na wadau wa maendeleo na watendaji wa TASAF inayonyesha kuwa kumekuwa na mafanikio makubwa katika shughuli za Mpango ambapo walengwa wameonyesha kuridhishwa na namna huduma za Mpango huo zinavyowanufaisha hususani katika Nyanja za elimu, afya,lishe na kuamsha ari ya kukuza shughuli za uzalishaji mali kwenye maeneo ya walengwa.
Vikao kazi hivyo vinatarajiwa kukamilika Ijumaa ya wiki hii kwa kufikia makubaliano ya namna ya kuboresha Zaidi shughuli za Mpango wa kunusuru kaya maskini.