Mwenyekiti
wa Mtandao wa Kimataifa wa Wabunge (PGA) Mhe. Pindi Chana ( MB)
akimkabidhi Rais wa Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa, Bw.Mogens
Lykketoft,Tamko la wabunge lenye sahihi 607 za wabunge kutoka mataifa
70 la kutokomeza ndo za utotoni na za kulazimisha katika hafla fupi
iliyofanyika Umoja wa Mataifa siku ya Jumatatu.
Mwakilishi
wa Kudumu wa Zambia katika Umoja wa Mataifa, Balozi Dr. Mwaba
Kasese-Bota akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo alianisha mipango
mbalimbali inayofanywa na serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
wakiwamo viongozi wa kimila katika kuzunguia ndoa za utotoni na za
kulazimishwa.
Mwakilishi
wa Kudumu wa Ghana katika Umoja wa Mataifa, Balozi Martha Anna Akyaa
Pobea naye akitoa mchango wa namna gani serikali yake
inavyolishughulikiwa tatizo za ndoa za utotoni ambapo amesema katika
nchi za Afrika Magharibi katika kila watoto watano wa kike, wawili
huolewa kabla ya kutimiza miaka 18 na kwamba ndoa hizo za utotoni si
tu kwamba zinadumaza ukuaji wake lakini pia zinachaniga mimba za umri
mdogo, vifo vitokanavyo na uzazi, maambukizi ya magonjwa mbalimbali na
kuchangia umaskini kwa watoto wengi wa kike.
Sehemu
ya washiriki wa hafla hiyo wakiwamo watalamu kutoka Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wakiongozwa na Kaimu Katibu Mkuu,
Bi, Nuru Milao.
Na Mwandishi Maalum, New York
Mtandao
wa Kimataifa wa Wabunge kutoka Mabunge mbalimbali Duniani
(PGA), umemkabidhi Rais wa Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa Bw.
Mogens Lykketoft, tamko la kukomesha ndoa za utotoni na za
kulazimishwa kwa watoto wa kike.
Akikabidhi
tamko hilo lenye sahini Zaidi ya 607 kutoka nchi 70 Mwenyekiti wa
Mtandao huo wa wabunge, Mhe. Pindi Chana na ambaye pia ni Naibu Waziri
wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto amesema, kukabidhiwa kwa
tamko hilo kwa Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kunakwenda
sambamba na maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike
ambayo huadhamishwa kila Octoba ya mwaka.
Mwenyekiti
wa PGA, amesema wakati wa hafla hiyo fupi iliyofanyika hapa Umoja wa
Mataifa, siku ya Jumatatu kwamba, ushirikiano wa wadau mbalimbali
hasa wabunge , serikali na asasi za kiraia ni muhimu sana ikiwa
jumuiya ya kimataifa inataka kuondokana na kumaliza tatizo la ndoa za
utotoni na za kulazimishwa.