
Staa wa Hip Hop Bongo, Joseph
Haule 'Prof. Jay' akihamasisha wananchi kujitokeza kwenda kujiandikisha
"NDUGU ZANGU WANA WA ARUSHA NA TANZANIA KWA UJUMLA TUJITOKEZE
KUJIANDIKISHA ILI TUJIHAKIKISHIE UHURU WA KWELI NA SIYO MATUMAINI"
Mbuge wa Arumeru Mashariki,
Mh. Joshua Nassari amewataka Watanzania kutambua muda wa mateso
waliyoyapata kwa miaka mingi sasa yamefikia ukomo,"Njia pekee iliyobaki
ndugu zangu ni kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura."

Mbuge wa Arumeru Mashariki, Mh. Joshua Nassari akionyesha magari mawili ya wagonjwa 'ambulance' alizozitoa kwenye jimbo lake.
![]() |
| Mjumbe wa Kamati Kuu na Mbunge wa Viti Maalum Mh. Grace Kiwelu aliwataka wanawake kuwa chachu ya mabadiliko kwa Taifa."MUDA WA KUDANGANYWA KWA KANGA UMEPITA TUJITOKEZE KUJIANDIKISHA ILI OKTOBA TUPATE UHURU WA UHAKIKA,WANAWAKE TUKIAMUA TUNAWEZA" |


Mbunge wa Arusha Mjini, Mh.
Godbless Lema ambaye pia ndiye aliyeteuliwa na chadema Kanda ya
Kaskazini kuwa kiongozi wa kampeni za hamasa ya kujiandikisha aliwaambia
wananchi wa Arusha kuwa safari ndiyo imeanza sasa kuelekea majimbo yote
33 ya kanda ya kaskazini kuhakikisha Watanzania wanajiandikisha kwa
wingi ili Oktoba wafanye maamuzi sahihi.


Mbunge wa Rombo, Joseph
Selasini "WATANZANIA WENZANGU HUU NDIYO MUDA MUAFAKA WA KILA MMOJA WETU
KUJIANDIKISHA ILI IKIFIKA OKTOBA TUWE TUNAFANYA MAAMUZI YA UHAKIKA NA
SIYO SAFARI YA MATUMAINI"

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa
Manyara, Mh. Pauline Gekul aliwataka Watanzania kujiandikisha na
kuhamasishana kwa wingi kwa kutumia simu, mitandao ya kijamii na vikao
vya kijamii ili ifikapo Oktoba waiondoe CCM madarakani.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa
Arusha Mh Cecilia Daniel Paresso amewataka Vijana na Akina Mama
kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha ili ikifika October waweze
kufanta maamuzi ya UHAKIKA na sio ya maamuzi ya MATUMAINI.
![]() |
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha Mh Rebecca Mgodo
amewataka wananchi kusoma nyakati"NDUGU ZANGU MIAKA YA MATESO KWA
WATANZANIA SASAS IMEFIKA MWISHO, TWENDENI KWA UMOJA WETU TUKAJIANDIKISHE KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURATUITOE CCM MADARAKANI"-Mgodo![]() |
Mwenyekiti wa Chadema Kanda Ya
Kaskazini Mh Israel Natse akiwaongoza viongozi na Wabunge wa Chadema
Kanda ya Kaskazini kuingia uwanjani huku wakiwapungia wanachama na
wapenzi wa Chadema waliofika uwanjani vya kilombero (PICHA NA WOINDE
SHIZZA)




