Waziri wa Michezo wa Afrika Kusini,
Fikile Mbalula, amesema rais wa zamani wa Afrika kusini, Thabo Mbeki,
ndiye aliyeruhusu ulipwaji wa dola milioni 10 kwa FIFA, hela ambazo sasa
zinadaiwa zilikuwa rushwa.
Serikali ya Afrika Kusini imekuwa
ikisisitiza kwamba fedha hizo zilikuwa ni sehemu ya mchango wa kusaidia
kukuza soka katika nchi za Caribbean lakini waendesha mashtaka wa
Marekani wanadai kitita hicho kilitolewa kama hongo kushawishi FIFA
kutoa haki ya kuandaliwa mashindano ya kombe
la dunia ya 2010 katika
nchi hiyo.
Mbeki mwenyewe hajatoa kauli yoyote
kuhusiana na swala hilo. Barua inayosemekana iliandikwa na shirikisho la
soka nchini Afrika kusini, inaonekana kuongeza uzito kwenye shutuma
kwamba serikali ya nchi hiyo ilitoa malipo hayo kwa siri.
Madai ya ufisadi dhidi ya Shirikisho
la Soka Duniani (FIFA) wamelitikisha shirikisho hilo na hata kupelekea
rais wake, Sepp Blatter kujiuzulu ghafla ikiwa imepita wiki moja tu
tangu achaguliwe tena kuongoza kwa miaka minne.
CHANZO: IRAN SWAHILI