May 4, 2015

Maalim Seif Sharif achangiwa fedha za kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya urais wa zanzibar wakati utakapofika

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad,akipokea fedha taslim kiasi cha shilingi milioni mbili na laki tano, kutoka kwa Mwenyekiti wa CUF zoni ya Mjini Unguja, Massoud Khamis, ili aweze kuchukua fomu ya kugombea urais wa Zanzibar wakati utakapofika.
Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akionyesha fedha alizokabidhiwa kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea urais.
Mwenyekiti wa CUF zoni ya Mjini Unguja, Massoud Khamis, akimkabidhi Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, cheti cha heshima kutokana na uongozi wake.
Baadhi ya viongozi na wanachama wa CUF waliojitokeza katika hafla ya kumkabidhi fedha Maalim Seif iliyofanyika nyumbani kwake Mbweni. (Picha na Salmin Said, OMKR)