
Watu
kadhaa wamepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa asubuhi hii kwenye
ajali ya basi la Wibonela lililokuwa likitoka Kahama kwenda Dar
lililopinduka eneo la kona ya Phantom, Kahama.
Chanzo cha
ajali hiyo ni mwendo kasi uliopelekea dereva wa basi kushindwa kulimudu
lilipofika kwenye kona ya Phantom na kupelekea kuingia mtaroni na
kupinduka.

Baadhi ya
miili tayari imetolewa katika eneo la ajali huku majeruhi nao
wakikimbizwa kwenye Hospitali ya Wilaya Kahama kwa matibabu.
Katika hatua nyingine, mtu mmoja amechomwa moto na wananchi wenye hasira kali baada ya kunaswa akiwaibia Majeruhi badala ya kutoa msaada.
Katika hatua nyingine, mtu mmoja amechomwa moto na wananchi wenye hasira kali baada ya kunaswa akiwaibia Majeruhi badala ya kutoa msaada.



