Taarifa hiyo pia imeshusha kigezo kwa waombaji wenye Full Technician Certificate (FTC) kutoka wastani wa B hadi kufikia wastani wa C.
Aidha TCU imewatangazia watu wote wenye uhitaji wa kuendelea na vyuo vikuu wenye GPA ya 3.0 kwa Stashahada na wastani wa C kwa wenye FTC watume maombi kupitia TCU kabla ya Septemba 23, mwaka huu.
Pia TCU imesema kuwa wale ambao walikuwa tayari wamekwishatuma maombi, na wanakidhi vigezo hivi hawatakiwi kuomba tena.