
Dkt.
Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli wameweka mashada ya maua katika
Kaburi la Marehemu Dkt. Omar Ali Juma na wameshiriki Dua ya kumuombea
Marehemu iliyoongozwa na Viongozi wa Madhehebu ya Dini ya Kiislamu na
Kikristo.

Akizungumza
mara baada Dua, Rais Magufuli amesema anamkumbuka Marehemu Dkt. Omar
Ali Juma kwa ukarimu wake, upendo, kutojikweza, kutobagua watu na
kudumisha amani katika siku zote za maisha yake.
Dkt. Magufuli ametoa wito kwa Watanzania kudumisha kwa vitendo amani aliyoisimamia Marehemu Dkt. Omar Ali Juma.
“Mimi najua huko aliko Marehemu Dkt. Omar Ali Juma anaendelea
kuliombea Taifa hili ili hiyo amani aliyoihubiri katika maisha yake, ili
huo upendo aliousimamia katika maisha yake, ili huo uchapa kazi kwa
ajili ya manufaa ya watanzania wote tuweze kuendeleza kwa mioyo yetu
yote” Amesema Rais Magufuli.
Rais
Magufuli akiweka shada la maua katika Kaburi la Marehemu Dkt. Omar Ali
Juma Makamu wa Rais wa zamani katika awamu ya Tatu katika kijiji cha
Wawi Bigilini katika Wilaya ya Chake chake Pemba.

Mama
Janeth Magufuli akiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Dkt.
Omar Ali Juma Makamu wa Rais wa zamani kijiji cha Wawi Bigilini kisiwani
katika Wilaya ya Chake chake Pemba.
Rais Magufuli akitazama kikundi cha ngoma baada ya kutua Pemba
ambapo pia ameenda kuzulu kaburi la aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk Omary
Ali Juma. Baadaye saa tisa alasiri atafanya mkutano wa hadhara katika
uwanja wa Gombani ya Kale, Pemba. Picha na Ikulu