Madalali wa Shirika la Nyumba la
Taifa (NHC) wamefika katika ofisi za gazeti la Tanzania Daima zilizopo
jengo la Klabu maarufu jijini Dar, Bilicanasa, leo asubuhi na kuanza
kuondoa vifaa ofisini hizo kutokana na deni la pango la mmiliki wa
gazeti hilo, Freeman Mbowe.
Mhariri
Mtendaji wa Tanzania Daima, Neville Meena amethibitisha hayo na kusema
kuwa kwa sasa wako kwenye msukosuko mkubwa lakini wanafanya jitihada za
kukabiliana na hali hiyo ili kuhakikisha uzalishaji wa gazeti unafanyika
kama kawaida.
Siku
za hivi kaibuni, Mkurugenzi wa NHC, Bw. Nehemia Mchechu alimtaja Mbowe
kama miongoni mwa wadaiwa sugu wa shirika hilo na kudai alishamuandikia
notisi yakulipa deni notisi ambayo imeisha jana.
Inasemekana pia kuwa, Klabu ya Bilicanas nayo ipo hatarini kufungwa kutokana na deni la pango.