Jul 29, 2016

Advans Bank sasa yawa rasmi Letshego Bank (T) Limited


Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Letshego ya Tanzania Bw. Yohane Kaduma (wa pili kulia) akionyesha nembo na muonekano mpya ya benki hiyo iliyobadilishwa kutoka kutambulika kama Advans Bank kuwa rasmi Letshego Bank. Wanaoshuhudia ni Dru Jayaratne (wa kwanza kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa FAIDIKA Bw. Mbuso Dlamini (wa pili kushoto) na Meneja Rasilimali watu wa benki ya Letshego Bi. Rehema Ngusar. 
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Letshego ya Tanzania Bw. Yohane Kaduma akiomwonyesha Mkurugenzi Mtendaji wa FAIDIKA Bw. Mbuso nembo na muonekano mpya ya benki hiyo iliyobadilishwa kutoka kutambulika kama Advans Bank kuwa rasmi Letshego Bank. 

Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Letshego ya Tanzania Bw. Yohane Kaduma (wa pili kulia) akipongezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa FAIDIKA Bw. Mbuso Dlamini (wa pili kushoto) mara baada ya kuzindua nembo na muonekano mpya ya benki hiyo iliyobadilishwa kutoka kutambulika kama Advans Bank kuwa rasmi Letshego Bank. Wanaoshuhudia ni Dru Jayaratne (wa kwanza kulia), na Meneja Rasilimali watu wa benki ya Letshego Bi. Rehema Ngusar. 
 Benki ya Advans ya Tanzania imebadili jina kuwa Letshego Bank (T) Limited kufuatia umiliki wa asilimia 75 za hisa za benki hiyo iliyonunuliwa na kampuni ya Letshego Holdings Limited baada ya kuwekeza zaidi ya Shilingi bilioni 19.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa muonekano mpya wa benki hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bw. Yohane Kaduma alisema umiliki huu uliyofanyika tangu mwaka 2015, umefanya Letshego kuwa mbia mkuu wa benki hiyo huku asilimia 25 ikiendelewa kumilikiwa na wanahisa waanzilishi ambao ni Advans SA, na Shirika la Maendeleo ya Uholanzi (FMO) ambao kwa mujibu wa Bw. Kaduma, watendelea kutoa ushirikiano kiuongozi na kiutawala.
Bw. Kaduma aliongeza kuwa pamoja na kuzindua muonekano mpya wa benki hiyo, Letshego ya Tanzania pia imezindua safari ya mabadiliko itakayoiwezesha kuwa kinara katika kuvumbua na kutoa huduma za kifedha ambazo ni shirikishi kwa wanajamii wote (financial inclusion).
Alisema uboreshwaji wa huduma zitakazotolewa na benki hiyo inalenga kusaidia katika kutatua matatizo muhimu ya wateja wao ambayo ni pamoja na kuweka amana, kukopa, kufanya malipo na hata huduma za bima.
“Mwonekano huu mpya wa Letshego Bank ni badiliko ambalo linafanyika katika nchi zote 10 barani Afrika ambapo tupo, na unazindua upya safari ya mabadiliko inayochukuliwa na Letshego. Kwa Tanzania, mabadiloko tuliyoyafanya kama benki, yanaendana pia na dira ya Serikali ya kuleta mendeleo ya kiuchumi na huduma za jamii kwa wananchi wake,” alisema Bw. Kaduma.