Kiongozi Mkuu wa ACT Zitto Kabwe
amejitokeza leo kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho, Kijitonyama
jijini Dar es Salaam baada ya taarifa kutolewa jana na chama chake kuwa
hawajui alipo tangu juzi Jumamosi juni 11.
Akizungumza na wanahabari leo baada ya
kujitokeza, Mh. Zitto Kabwe amesema kuwa hatishiki na vitisho
vinavyotolewa na Jeshi la Polisi nakwamba amekusudia kufanya kongamano
la kujadili bajeti kesho Makao Makuu ya Chama hicho huku akiitaka jeshi
la Polisi kuacha kumvizia na badala yake limkamate kwa kufuata Sheria