

Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na Makamanda wa Polisi, Wanasheria wa Serikali, Wafawidhi wa Mikoa na
Wakuu wa upelelezi wa Mikoa na Vikosi kabla ya kufungua rasmi Kikao kazi
cha Makamanda hao wa Polisi katika Ukumbi wa Dodoma Convention Center.

Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
amesimama pamoja na viongozi wengine wakati wimbo wa Jeshi la polisi
ukipigwa. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Charles
Kitwanga, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana, Mwanasheria Mkuu wa
Serikali George Masaju, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Valentino Mlowola,
Kushoto kwake ni Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harison Mwakyembe ,
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Yusuph Masauni na
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Ernest Mangu.

Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili
kwenye ukumbi wa Mikutano wa Dodoma Convention Center kwa ajili ya
ufunguzi wa rasmi Kikao kazi cha Makamanda hao wa Polisi.

Baadhi
ya Makamanda wa polisi wa Mikoa mbalimbali wakipiga makofi wakati Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa
akiwahutubia.