
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imefarijaka kwa ushindi wa
wasanii wa filamu nchini walioshinda tuzo za filamu Afrika za mwaka
2016 (African Magic Viewers Choice Award) ziliyofanyika jijini Lagos
nchini Nigeria mwishoni wa wiki iliyopita.

Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea Tuzo kutoka kwa Msanii wa filamu
Elizabeth Michael ambayo msanii huyo alishinda nchini Nigearia. Tukio
hilo lilifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Machi 11,
2016.

Waziri
Mkuu, Kasim Majaliwa akipokea tuzo kutoka kwa msanii wa filamu, Single
Mtambalike ambayo msanii huyo alishinda nchini Nigeria. Tukio hilo
lilifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Machi 11, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imefarijaka kwa
ushindi wa wasanii wa filamu nchini walioshinda tuzo za filamu Afrika
za mwaka 2016(African Magic Viewers Choice Award) ziliyofanyika jijini
Lagos nchini Nigeria mwishoni wa wiki iliyopita.
Waziri Mkuu Majaliwa, amesema hayo leo katika ukumbi wa mikutano
ulipo katika Ofisi yake Jijini Dares Salaam, alipokutana na washindi
wa tuzo za filamu Afrika za mwaka 2016 (AMVCA) ambao ni Elizabeth
Michael ‘Lulu’ aliyeshinda tuzo ya Filamu Bora ya Afrika Mashariki na
Single Mtambalike ‘Richie’ aliyeshinda tuzo ya Filamu Bora ya Kiswahili
pamoja Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Mhe.
Annastazia Wambura,Katibu Mkuu wa wizara Habari,Utamaduni,Sanaa na
Michezo, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bi Joyce Fisso na
wasanii wa filamu.
“Serikali imefarijika sana kwa nyie kwenda Nigeria na kushinda
na mmetumia lugha ya Kiswahili, lazima tutumie nafasi hii kuwatangaza
pia mmuendelee na fani hii ili kuvutia wengi zaidi” amesema Waziri Mkuu Majaliwa.
Aidha, Waziri Mkuu amewapongeza wasanii hao na kusema kuwa
Serikali itaendelea kushirikiana na wasanii wakati wowote na amewataka
kujipanga vizuri kutumia vyama vyao vya sanaa na kusisitiza kuwa Mhe.
Rais John Pombe Magufuli ametoa matamko kadhaa kuhusu sanaa na
wasanii na ameendelea kushughulikia malalamiko yao ikiwemo suala la
COSOTA, na kusema kuwa baada ya taratibu zote kukamilika suala hilo
litasimamiwa na Wizara inayohusika na kazi za Sanaa.
Waziri Mkuu Majaliwa, pia amewataka watanzania kuacha tabia ya
kutojiamini na kujidharau, na kuwataka watu waige mfano kwa wasanii
hao, na kuwashauri wasanii wote kwa ujumla kutumia vyombo vya habari
kujiimarisha na kujitangaza.
Kwa upande wao, wasanii waliopata tuzo hizo kwa filamu ya
“mapenzi ya Mungu” ya Elizabeth Michael na filamu ya “Kitendawili” ya
Single Mtambalike, wameishukuru Serikali kwa kuwathamini na kuonesha
ushirikiano katika kazi zao za sanaa, na wameahidi kuendelea
kutengeneza kazi nzuri za sanaa ili ziweze kuitangaza Tanzania
kimataifa.
Naye, Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania(TAFF) Saimon Mwakifamba
ameishukuru Serikali kwa jitihada mbalimbali inazofanya katika
kusaidia tasnia ya sanaa kwa ujumla na ameahidi kuendelea kushirikiana
na Serikali katika kuendeleza tasnia hiyo kimataifa.