Waziri
wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
akizungumza katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya sekta ya afya
unaofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, wadau hao wa
Sekta ya afya wanajadiliana mambo mbalimbali na baada ya kumalizika kwa
mkutano huo kutakuwa na kusaini makubaliano yaliyofikiwa kwa
utekelezaji katika sekta ya afya hapa nchini , Katika picha kulia ni
Carol Hannon Mshauri wa Afya katika ubalozi wa Ireland nchini Tanzania.
Carol
Hannon Mshauri wa Afya katika ubalozi wa Ireland nchini Tanzania
akizungumza katika mkutano huo Kushoto ni Waziri wa Afya, Ustawi wa
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu.
Dk.Ulisubisya
Mpoki Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto akichangia hoja katika mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa
Karimjee jijini Dar es salaam.
Dk.
Deo Mtasiwa Naibu Katibu Mkuu wa Afya TAMISEMI akizungumza katika
mkutano huo ambao umekutanisha wadau wa afya na kujadili changamoto
mbalimbali zinazokabili sekta ya afya.
Baadhi ya wadau wakiwa katika mkutano huo.