Meneja
wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro Eng. Dorothy Ntenga
akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame
Mbarawa namna maji yanavyopiga kingo za daraja la Dumila wakati Waziri
huyo akikagua ujenzi wa kingo mpya zinazojengwa kudhibiti mafuriko hayo.
Meneja
wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Dodoma Eng. Leornad Chimagu
(kulia),akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Profesa Makame Mbarawa kuhusu athari za mafuriko katika kingo za
barabara ya Gairo-Dodoma eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma.
Muonekano
wa Daraja la Dumila mkoani Morogoro lilivyo sasa kufuatia mvua
zinazonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kusababisha mafuriko
yanayoelekea katika Mto Mkondoa.
Mafundi
wakiendelea na ujenzi wa kingo za barabara zilizo athiriwa na mvua
zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kusababisha
uharibifu wa barabara katika eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma.