Jan 29, 2016

PROFESA MBARAWA AKAGUA ATHARI ZA BARABARA MORO – DODOMA.

 Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro Eng. Dorothy Ntenga akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa namna maji yanavyopiga kingo za daraja la Dumila wakati Waziri huyo akikagua ujenzi wa kingo mpya zinazojengwa kudhibiti mafuriko hayo.
 Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Dodoma Eng. Leornad Chimagu (kulia),akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu athari za mafuriko katika kingo za barabara ya Gairo-Dodoma eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma.
 Muonekano wa Daraja la Dumila mkoani Morogoro lilivyo sasa kufuatia mvua zinazonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kusababisha mafuriko yanayoelekea katika Mto Mkondoa.
 Mafundi wakiendelea na ujenzi wa kingo za barabara zilizo athiriwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma na kusababisha uharibifu wa barabara katika eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma.