Jan 26, 2016

DK SHEIN ASHIRIKI MAZISHI YA MAREHEMU RAMADHANI NYONJE PANDU ZANZIBAR.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein na Viongozi na Wananchi wakishiriki katika Sala ya kumsalia marehemu Ramadhani Nyonje Pandu iliofanyika katika msikiti wa fuoni na kuzikwa kijijini kwao Paje Wilaya ya Kusini Unguja.(Picha na Ikulu).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akishiriki dua ya kuuombea Mwili wa Marehemu Ramadhani Nyonje Pandu wakati alipofika nyumbani kwa marehemu fuoni michezani Unguja kutoa mkono wa pole kwa wanafamilia leo asubuhi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akimfariji Mjane wa Marehemu Ramadhani Nyonje Panda alipofika nyumbani kwao fuoni michezani kutowa mkono wa pole kwa wana familia, kulia Kadhi Mkuu wa Zanzibar Shekh Khamis Haji Khamis.
WANANCHI wakiwa katika msiba wa marehemu Ramadhani Nyonje Pandu aliyewahi kuwa Mwakilishi wac Jimbo la Muyuni Zanzibar.
WANANCHI wakiwa katika msiba wa marehemu Ramadhani Nyonje Pandu wakiwa nyumbani kwa marehemu fuoni michezani Unguja wakisubiri taratibu za mazishi ya marehemu kupelekwa kijiji kwao Paje kwa mazishi.