Matokeo ya uchunguzi huo ya Uholanzi yatatolewa leo.
Yan Novikov, kiongozi wa shirika hilo la Russia liitwalo Almaz-Antey, akizungumza na waandishi wa habari hakufafanua kilichokuwa katika ripoti hiyo na hakusema iwapo alidokezwa kilichokuwemo ndani yake.
Ndege hiyo ilianguka Julai 17, 2014, katika eneo linaloshikiliwa na waasi mashariki mwa Ukraine na inaaminika ilipigwa na kombora lililotoka ardhini kwenda angani.
Ukraine na nchi za Magharibi zinasema kombora hilo lilifyatuliwa na majeshi ya Russia au waasi wanaoungwa mkono na Russia.
chanzo:GPL