Mke
wa Rais na Mwenyekiti wa Bodi ya WAMA, Mama Salma Kikwete akipokewa na
Mkuu wa Wilaya ya Lindi Ndugu Yahaya Nawanda baada ya kuwasili kwenye
eneo la Shule ya Sekondari ya Wasichana WAMA Sharaf huko Lindi Mjini
kwenye sherehe ya uzinduzi rasmi wa shule hiyo tarehe 11.10.2015.
Rais
Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na Bwana Ibrahim Sharaf, Rais wa Sharaf
Group of Companies ya nchini Dubai mara baada ya kuwasili kwenye Shule
ya Sekonadi ya Wasichana WAMA Sharaf huko Lindi. Rais Kikwete alikuwa
mgeni rasmi katika sherehe ya uzinduzi wa Shule hiyo tarehe 11.10.2015.
Rais
Dkt. Jakaya Kikwete akiondoa kitambaa kwa kushirikiana na Bwana Ibrahim
Sharaf aliyefadhili ujenzi wa Shule ya Wasichana ya WAMA Sharaf ikiwa
ni ishara ya kuizindua rasmi. Baadaye Rais Dkt. Kikwete akishirikiana na
viongozi wengine walisaidia ujenzi wa shule hiyo kukata utepe ikiwa ni
mwendelezo wa sherehe za ufunguzi rasmi wa shule hiyo huko Lindi tarehe
11.10.2015.