Waandishi wa habari wa
kimsikiliza Mkurugenzi wa Matibabu na Huduma za kiufundi Dr. Frank Lekey kikao hicho kimefanyika leo jiji Dar es
Salaam
(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)
MFUKO
wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ni Taasisi ya umma iliyoanzishwa kwa Sheria
Namba 8 ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1999, ikiwa na
jukumu la kusimamia huduma za matibabu kwa wanachama na wategemezi wao kupitia
vituo vya ngazi mbalimbali za matibabu ( zahanati, vituo vya afya, hospitali na
maduka ya dawa). Mfuko ulioanza kutoa
rasmi huduma kwa wanachama wake Mwezi Oktoba, 2001.
Katika kipindi cha miaka kumi ya
uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, dokta Jakaya Kikwete, Mfuko
umepiga hatua kubwa ya maendeleo kama inavyoelezwa hapa chini:
Takwimu za mafanikio katika kipindi cha miaka kumi (2005 hadi 2015)
katika maeneo mbalimbali ni kama ifuatavyo:
Usajili wa Wanachama wa NHIF na CHF.
A: Wanachama wa NHIF
|
SN
|
MWAKA 2005
|
MWAKA 2015
|
Ongezeko la Asilimia
|
|
1
|
Idadi
ya wanachama Wachangiaji 275,865
|
Idadi
ya Wanachama Wachangiaji 640,341
|
132
|
|
2
|
Idadi
ya Wanufaika 1,268,979
|
Idadi
ya Wanufaika 3,237,434
|
155
|
B: Wanachama
wa CHF:
|
SN
|
MWAKA 2009
|
MWAKA 2015
|
Ongezeko la Asilimia
|
|
1
|
Halmashauri
zilizotekeleza 99
|
Halmashauri
zinazotekeleza 144
|
87%
|
|
2
|
Idadi
ya Kaya 120,000
|
Idadi
ya Kaya 1,112,874
|
927%
|
|
3
|
Idadi
ya Wanufaika 720,000
|
Idadi
ya Wanufaika 6,677,244
|
927%
|
Hivyo
hadi kufikia Juni 2015 jumla ya wanufaika wa NHIF na CHF ni 9,914,678 ambayo ni
sawa na asilimia 22.8 ya Watanznaia wote kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012.
Jukumu lingine la NHIF ni kusajili vituo vya matibabu
ambapo wanachama na wategemezi wao wanakwenda kupata huduma, katika kipindi cha
miaka kumi, takwimu za usajili ni kama ifuatavyo:
|
Maelezo
|
2005/06
|
2011/12
|
2012/13
|
2013/14
|
2014/15
|
|
Zahanati
|
3,346
|
4,240
|
4,513
|
4,621
|
4,744
|
|
Vituo vya Afya
|
385
|
549
|
591
|
605
|
614
|
|
Hospitali
|
200
|
234
|
238
|
246
|
254
|
|
Maduka ya Dawa
|
36
|
143
|
169
|
178
|
202
|
|
Maduka ya Dawa Muhimu
|
-
|
260
|
326
|
358
|
361
|
|
Kliniki za Vipimo
|
-
|
-
|
2
|
3
|
8
|
|
Vituo vya Uchunguzi
|
-
|
-
|
1
|
1
|
2
|
|
Jumla
|
3,967
|
5,426
|
5,840
|
6012
|
6,185
|
Malipo kwa Watoa Huduma:
Jukumu
lingine la NHIF ni kuwalipa watoa huduma, ambapo
tangu mwaka 2005 hadi kufikia Juni 30,
2015, jumla ya Shilingi Bilioni
555,008.80 zimelipwa kwa watoa huduma. (Zahanati, Vituo vya Afya,
Hospitali, Vituo vya Uchunguzi na maduka ya dawa).
Mahudhurio katika vituo vya matibabu:
Katika
kipindi cha miaka kumi cha kuanzia 2005
hadi 2015 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umelipia mahudhurio 27, 394,173 ya matibabu ya wanachama na
wategemezi wao katika vituo vilivyosajiliwa.
Mikopo ya Ukarabati, vifaa tiba, TEHAMA
na dawa:
Ili
kuboresha huduma Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulianza kutoa mikopo ya ukarabati
wa majengo, vifaa tiba, TEHAMA na dawa tangu mwaka 2007.
Katika kipindi cha miaka nane tangu
mwaka 2007 hadi 2015 mikipo iliyotolewa ni kama ifuatavyo:
|
SN
|
AINA
YA MIKOPO
|
IDADI
YA VITUO
|
JUMLA
YA FEDHA
|
|
1
|
Ununuzi wa Vifaa Tiba
|
162
|
6.912 Bilioni
|
|
2
|
Ukarabati wa Majengo
|
36
|
4.120 Bilioni
|
|
|
Jumla
|
198
|
11.032 Bilioni
|
Miradi ya Uboreshaji wa Huduma za
Matibabu:
Serikali
ya Awamu ya Nne kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umeanza ujenzi wa Kituo
cha Kisasa cha Matibabu katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Kituo cha Mfano
cha Matibabu katika Hospitali ya mkoa wa Dodoma na majengo pacha katika Taasisi
ya Tiba za Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI). Matarajio ya Serikali ya Awamu ya
Nne ni kwamba miradi hii itapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto mbalimbali
zinazoikakabili sekta ya Afya nchini.
Huduma za Madaktari Bingwa.
Tangu
mwaka 2012 Mfuko umeanza mpango
kabambe wa kuwapeleka MADAKTARI BINGWA
katika maeneo ya pembezoni mwa nchi yetu kwa ajili ya kutoa huduma maalumu.
Hadi kufikia Juni 30, 2015 Mfuko
umetoa huduma hizo katika mikoa ya Lindi,
Kigoma, Pwani, Rukwa, Katavi, Manyara, Tabora, Mtwara, Shinyanga, Simiyu na
Mara ambapo zaidi ya wananchi 9,232 walihudumiwa
katika maeneo hayo na zaidi ya wananchi 370
walifanyiwa upasuaji wa aina mbalimbali katika mikoa iliyotembelewa.
Madaktari
bingwa walioshiriki katika zoezi hili walitoka katika Hospitali ya Taifa wa
Muhimbili, Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) Hospitali ya
Rufaa ya Mbeya na Hospitali ya Rufaa ya Bugando. Madaktari hao ni mabingwa wa
magonjwa ya moyo, magonjwa ya wanawake, magonjwa ya watoto, magonjwa ya ndani,
magonjwa ya figo, wataalamu wa upasuaji na dawa za usingizi na huduma za
wagonjwa mahututi.
KAULI MBIU YETU: HUDUMA BORA ZA
MATIBABU NI HAKI YAKO NI DHAMANA YETU.