Mke
wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi,CCM, Mama
Salma Kikwete akimnadi mgombea Urais kupitia CCM, Mheshimiwa Dkt. John
Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa
Mpilipili huko Lindi Mjini tarehe 12.10.2015.
Mgombea
Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza
Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC, Mama Salma Kikwete mara baada ya kumwombea
kura kwa wananchi wa Manispaa ya Lindi kwenye mkutano wa kampeni
uliofanyika kwenye uwanja wa Mpilipili tarehe 12.10.2015. Aliyesimama
kulia ni Mgombea Ubunge katika Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye.
Mke
wa Rais na Mjumbe wa NEC Mama Salma Kikwete akiwa katika kijiji cha
Ngunichile kilichoko katika Wilaya ya Nachingwea kwa ajili ya kuwanadi
wagombea wa Chama Cha Mapinduzi kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika
tarehe nchini tarehe 25.10.2015. Katika mikutano hiyo Mama Salma
alimnadi Dkt. John Magufuli kwenye urais na Ndugu Hassan Elias Masala
kwenye Ubunge wa Jimbo la Nachingwea na Madiwani wote katika wilaya hiyo
tarehe 13.10.2015.