Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,
IGP Ernest Mangu akiwasha mshumaa kama ishara ya upendo katika kaburi la
hayati baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere mwishoni mwa wiki wakati
alipokuwa katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Mara.Kulia ni Kamanda wa
Polisi mkoa wa Mara, ACP Philip Kalagi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,
IGP Ernest Mangu akipokea mfano wa fimbo aliyokuwa akitumia Hayati Baba
wa Taifa Mwl.Julius Nyerere kutoka kwa Chifu wa kabila la wazanaki
Bw.Japhet Wanzagi wakati alipotembelea nyumbani kwa hayati baba wa Taifa
mwishoni mwa wiki wakati alipokuwa katika ziara ya kikazi katika mkoa
wa Mara.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,
IGP Ernest Mangu (kushoto) akimsikiliza Chifu wa kabila la wazanaki
Bw.Japhet Wanzagi wakati alipotembelea nyumbani kwa hayati baba wa Taifa
Mwl.Julius Nyerere mwishoni mwa wiki wakati alipokuwa katika ziara ya
kikazi katika mkoa wa Mara.Kulia ni mtoto wa Nyerere, Madaraka Nyerere.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,
IGP Ernest Mangu akizungumza na Mhifadhi Mkuu wa mbuga ya Serengeti Bw.
Willium Mwakilema (kulia) wakati alipokuwa katika ziara ya kikazi katika
mkoa wa Mara.Katikati ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, ACP Philip
Kalagi.(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)