Oct 6, 2015

IDARA YA UHAMIAJI YAWA BINGWA MICHUANO YA MPIRA WA PETE KLABU BINGWA TANZANIA

Nahodha Msaidizi wa Timu ya Mpira wa Pete wa Idara ya Uhamiaji,Juliana Mwakalemela  akimkabidhi Kikombe cha Ushindi katika Michuano ya Klabu bingwa wa mpira wa pete Tanzania,Kamishina wa Utawala na Fedha wa Idara ya Uhamiaji,Piniel Mgonja katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
 
Wanamichezo wa mpira wa pete wa idara ya uhamiaji wakisherekea kombe baada ya kufika Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji leo jijini Dar es Salaam.
Wanamichezo wakimsikiliza Kamishina wa Utawala na Fedha  wa Idara ya Uhamiaji,Piniel Mgonja (hayupo pichani) leo baada kukabidhi Kikombe cha Ushindi katika Michuano ya Klabu bingwa wa mpira wa pete Tanzania leo Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
TIMU ya Mpira wa Pete ya Idara ya Uhamiaji,imeibuka mshindi katika michuano ya mashindano ya Klabu bingwa wa mpira wa pete baada ya kuipiga timu ya Mbweni JKT iliyokuwa ikishikilia ubingwa huo.
 
Akizungumza baada ya kupokea kombe hilo ,Kamishina wa Utawala na Fedha wa Idra ya Uhamiaji,Piniel Mgonja  amewataka wachezaji wa timu hiyo kujituma na kuweza kulinda kombe hilo ililisichukuliwe katika michuano mingine.
 
Mgonja amesema katika mwaka huu wamekuwa wakishinda katika masuala mbalilmbali hivyo  kushinda huko inatokana na wafanyakazi kujituma kuaniza kutoa huduma hadi michezo.
 
Aidha amewataka wafanyakazi kuonyesha vipaji vyao katika michezo mbalilmbali ili kuweza kufanya vizuri katika michezo  na kuweza idara ya uhamiaji kuwa ni sehemu ya vipaji.
 
Nahodha wa timu hiyo wa Idara ya Uhamiaji,Nina Muliga ameitaka Idara kuwawezesha kuanzia viwanja pamoja na rasilimali fedha ili kuongeza ufanisi wa michezo mbalimbali wa kuleta ushindi.