Oct 13, 2015

BENKI YA NBC YATOA MSAADA KWA WALEMAVU WA NGOZI

 Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Mussa Jallow (wa tatu kushoto), akikabidhi pikipiki kwa Mwenyekiti wa Chama cha Albino (TAS) Mkoa wa Pwani, Thomas Diwani, katika hafla ambayo NBC ilikabidhi pikipiki tatu, kofia, miwani na mafuta ya ngozi ikiwa ni sehemu ya juhudi za benki hiyo katika kuisaidia jamii. Hafla ya makabidhiano ilifanyika Kibaha, Pwani jana. Wengine ni baadhi ya wanachama wa TAS na maofisa wa NBC.
 Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Kibaha, Asia Chambega (wa tatu kushoto) akikabidhi pikipiki kwa mmoja wawakilishi wa Chama cha Albino (TAS) Mkoa wa Pwani, Haika Ngowo, katika hafla ambayo NBC ilikabidhi pikipiki tatu, kofia, miwani na mafuta ya ngozi ikiwa ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuisaidia jamii. Hafla ya makabidhiano ilifanyika Kibaha, Pwani jana. Wengine kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa NBC, Alina Maria Kimaryo na Mwenyekiti wa TAS Mkoa wa Pwani, Thomas Diwani.
  Meneja Masoko wa Benki ya Taifa ya Biashara( NBC) Alina Maria Kimaryo (kushoto), akizungumza na baadhi ya wanachama wa Chama cha Albino (TAS) Mkoa wa Pwani  katika hafla ambayo NBC ilikabidhi pikipiki tatu, kofia, miwani na mafuta ya ngozi ikiwa ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuisaidia jamii katika kukuza uchumi na pia kujali afya zao. Hafla ya makabidhiano ilifanyika Kibaha mkoani Pwani jana.