Katibu
Mkuu wa TASOI, Belinda Mlingo akizungumza na waandishi wa habari(hawapo
pichani) wakati wa uzinduzi wa mpango mkakati endelevu wa kuendesha
kampeni ya Mshikamano dhidi ya Saratani kwa kutumia technolojia ya
mawasiliano bila malipo yoyote katika ukumbi wa Taasisi ya Saratani
Ocean Road leo jijini Dar.
Mshauri kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dk. Dominista Kombe ambaye akitoa takwimu ya wagonjwa wanaofika kutibiwa katika hospitali hiyo.
Mkurugenzi
wa Idara ya Kinga Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dk. Julius Mwaiselage
akizungumza jambo mbele ya waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati
wa uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Taasisi ya Saratani Ocean
Road leo.
Waandishi wa habari wakiendelea kuchuka habari.
Mkutano ukiendelea
ASASI
isiyo ya kiserikali ya Tanzania Social Outreach Initiative (TASOI),
imezindua kampeni rasmi mpango mkakati endelevu wa kuendesha kampeni ya
Mshikamano dhidi ya Saratani kwa kutumia teknolojia ya mawasiliano bila
malipo yoyote.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TASOI, Belinda Mlingo, alisema
kuwa kampeni hiyo itatoa elimu, uhamasishaji na kutoa ushauri nasaha
kwa wananchi kwa kupitia ujumbe mfupi wa simu (SMS).
Amesema
kuwa katika kampeni hiyo, TASOI inashirikiana na wadau mbalimbali
katika masuala ya afya, teknolojia na uhamasishaji wa jamii ili kutoa
huduma hii muhimu bila malipo au gharama yoyote kwa watumiaji wa simu za
mikononi.
“Kwa
kumnukuu Mkurugenzi Mkuu wa Kitengo cha Magonjwa ya Yasiyoambukiza
Wizara ya Afya, Profesa Ayoub Mgimba, ‘Hali halisi inadhihirisha kwamba
magonjwa yasiyoambukiza kama saratani hivi sasa yamekuwa ni tatizo kubwa
hasa katika nchi kama yetu ambapo ufahamu na mwamko ni mdogo sana juu
mazingira hatarishi, viashiria, matibabu na matunzo ya wahanga wa
magonjwa haya. Saratani inasababisha madhara makubwa ambayo yanaelekea
kuwa majanga kwa jamii na kiuchumi kwa Taifa.”