Mwenyekiti
wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (wa kwanza
kushoto) akiwa kwenye hali ya furaha mara baada ya kuzindua msimu wa
saba wa mbio za Rock City Marathon zinazotarajiwa kufanyika Novemba 15
mwaka huu katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Wengine ni pamoja
na Meneja Mkuu wa kampuni ya Capital Plus International (CPI) ambao ndio
warataibu wa mbio hizo Bw Erasto Kilawe (mwenye shati jeupe), Afisa
Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bw.
Salim Kimaro (wa pili kulia) na Bi Ummy Hassan kutoka idara ya Uhusiano
NSSF ambao ni moja wa wadhamini wakuu wa mbio hizo.
Meneja
Mkuu wa kampuni ya Capital Plus International (CPI) warataibu wa mbio
hizo Bw Erasto Kilawe (wa kwanza kushoto) akizungumza na waandishi wa
habari (hawapo kwenye picha) wakati wa uzinduzi wa msimu wa saba wa mbio
za Rock City Marathon zinazotarajiwa kufanyika Novemba 15 mwaka huu
katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Wengine ni pamoja na
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (wa pili
kushoto), Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya
Jamii (NSSF) Bw. Salim Kimaro (wa tatu kushoto).
Afisa
Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bw.
Salim Kimaro (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo
kwenye picha) wakati wa uzinduzi wa msimu wa saba wa mbio za Rock City
Marathon zinazotarajiwa kufanyika Novemba 15 mwaka huu katika Uwanja wa
CCM Kirumba jijini Mwanza. Wengine ni pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la
Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (wa kwanza kushoto) na Bi Ummy
Hassan kutoka idara ya Uhusiano NSSF ambao ni moja wa wadhamini wakuu wa
mbio hizo.
Na Mwandishi Wetu.
Mwenyekiti
wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi, amezindua msimu wa
saba wa mbio za Rock City Marathon zitakazofanyika Novemba 15 mwaka huu
kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mbio
za Rock City Marathon, zinazoandaliwa na Kampuni ya Capital Plus
International (CPI), kwa ushirikiano na Chama cha Riadha Tanzania (RT),
pamoja na Chama cha Riadha Mkoa wa Mwanza (MRAA) zinalenga kutambua na
kuinua vipaji vya wanariadha nchini na pia kukuza utalii wa ndani
kupitia sekta ya michezo.
Akizungumza
katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam, Bw.
Malinzi alisema baraza linafuraha kuona makampuni binafsi yakijiingiza
katika kuinua mchezo wa riadha nchini.
“Mchezo
wa riadha una changamoto kubwa na tunatambua jitihada zinazoendelea
kufanywa na kampuni ya Capital Plus katika kurudisha hadhi ya mchezo
huu nchini kama ilivyokuwa miaka ya sabini na themanini,” alisema.