Sep 6, 2015

MTANDAO WA WANAWAKE WAHITIMISHA TAMASHA LA UZINDUZI WA ILANI YA UCHAGUZI JIJINI DAR

 Mkurugenzi Mtendaji wa  Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi akizungumza na wananchi juu ya kutambua michango ya kimaendeleo inayofanywa na wanawake kwa kuwawekea kumbukumbu kama ilivyo kwa wanaume, ili kuleta uwiano wa kijinsia leo Jiji Dar es Salaam katika kilele cha tamasha la Jinsia.
 Mkurugenzi Mtendaji wa  Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi akiteta jambo na Ruth Meena.
 Wanawake wakitaja baadhi ya matatizo ambayo yanayowakabili ni pamaoja na suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama maeneo mbalimbali nchini.
Wanawake wameitaka tume ya taifa ya uchaguzi (NEC) kutofumbia macho suala la matusi na kejeli zinazofanywa na viongozi wa siasa katika kampeni zao.