
Wakazi
wa jiji la Dar es Salaam kutoka kushoto Anna Msinde, Mwanaidi Khaji na
Mariam Rajabu wakielekezwa na Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania, Athuman
Mwakipesile (kulia) jinsi ya kujiunga na huduma ya M-Pawa inayowawezesha
wateja wa kampuni hiyo kupata riba na mikopo ya bei nafuu kupitia simu
zao za mkononi wakati wa kongamano la wiki ya huduma za kifedha na
uwekezaji(Financial and Investment Service fair) lililofanyika katika
viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Mfanyakazi
wa Vodacom Tanzania, Athuman Mwakipesile (kushoto) akiwafafanulia jambo
baadhi ya wateja wa Vodacom Tanzania waliofika katika banda la kampuni
hiyo wakati wa kongamano la wiki ya huduma za kifedha na uwekezaji
(Financial and Investment Service fair) lililofanyika katika viwanja vya
Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Meneja
Mauzo wa Vodacom Tanzania kanda ya Mbagala jijini Dar es Salaam,Idd
Mawe akitoa semina ya mafunzo ya huduma ya M-pawa na M-pesa kwa Mawakala
na wateja wa kampuni hiyo wakati wa kongamano la wiki ya huduma za
kifedha na uwekezaji (Financial and Investment Service fair)
lililofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Baadhi
ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakitembelea mabanda ya Vodacom
Tanzania na kupatiwa mafunzo mbalimbali ya kujiunga na huduma ya M-Pawa
inayowawezesha wateja wa kampuni hiyo kupata riba na mikopo ya bei nafuu
kupitia simu zao za mkononi wakati wa kongamano la wiki ya huduma za
kifedha na uwekezaji(Financial and Investment Service fair)
lililofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
mwishoni mwa wiki.