Afisa
Mwandamizi anayeshughulikia Sera na maendeleo ya kilimo kutoka Taasisi
ya Kimataifa ya Bill na Melinda Gates Bw. Stanley Wood akizungumza na
waandishi wa Habari jijini Dar es salaam mara baada ya kufanyika kwa
kikao cha mazungumzo na viongozi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
nchini Tanzania kuangalia uwezekano wa taasisi hiyo kusaidia miradi ya
ukusanyaji wa Takwimu za kilimo nchini Tanzania.Kushoto kwake ni Mratibu
wa miradi wa Taasisi hiyo Bi.Bhramar Dey.
Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt.Albina Chuwa akizungumza na
waandishi wa habari Kuhusu umuhimu wa takwimu za Kilimo nchini Tanzania
na mikakati ya Serikali na wadau mbalimbali katika kufanikisha
upatikanaji wa Takwimu za kilimo nchini.Kulia kwake ni Mkurugenzi wa
Takwimu za Uchumi wa Ofisi hiyo Bw.Morrice Oyuke.
Mkuu
wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika Prof.Innocent Ngalinda
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mikakati ya chuo
anachokiongoza katika kutoa elimu kwa watakwimu wa kilimo nchini
Tanzania na mpango wa chuo hicho kuimarisha shughuli za ukusanyaji wa
takwimu za kilimo kwa kutumia wataalam wanaozalishwa.
Mtakwimu
mwandamizi kutoka Benki ya Dunia Bi.Elizabeth Talbert( kulia) na Meneja
wa Idara ya Viwanda na Ujenzi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi. Joy Sawe
wakifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya viongozi wa
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na wawakilishi wa Taasisi ya Kimataifa
ya Bill na Melinda Gates jijini Dar es salaam.Picha na Veronica Kazimoto.