Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa
PSPF, Ismail Juma(kushoto) akikabidhi jezi kwa kapteni wa timu ya G
Unity Fc kwa ajili ya mchezo wa fainali uliofanyika katika kiwanja cha
Kipunguni B katika kata ya Kipunguni manispaa ya Ilala jijini Dar.
Ambapo timu ya G Unity FC waliibuka washindi baada ya kuichapa timu ya
Sukuma Land Fc bao 5 kwa 2.
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa
PSPF, Ismail Juma(kushoto) akikabidhi jezi kwa kapteni wa timu ya
Sukuma Land FC wakati wa mchezo wa fainali wa kombe la Madereva bodaboda
wa kata ya Kipunguni.Wa pili kushoto ni ASP Mbunja Matibu kutoka Traffic Makao Makuu.
Mmoja wa Madereva Bodaboda akiendelea kupewa faida za mfuko wa Uchangiaji wa Hiari(PSS) kutoka kwa Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma(kushoto)
Mmoja wa madereva wa Bodaboda akijiunga kwenye mfuko
wa (PSPF) kupitia (PSS) ambapo kila mtu anaweza kujiwekea akiba kupitia
kwenye mfuko huo wa hiari wakati wa mchezo wa fainali.
Vijana waliofika katika mchezo wa fainali wakisoma vipeperushi vya mfuko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ambapo mfuko huo ulidhamini ligi hiyo iliyoendeshwa kwa wiki nzima
Mmoja wa Madereva Bodaboda akisoma maelekezo ya jinsi ya kutuma pesa kwenye akaunti kwenye mfuko wa Uchangiaji wa Hiari(PSS) mara baada ya kupatiwa kitambulisho cha uanachama wa mfuko wa PSPF.
Maafisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa
PSPF,waratibu wa michezo hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Timu ya
Sukuma Land ambapo katika mchezo huo timu hiyo iliibuka mshindi wa pili
baada ya kufungwa na timu ya G Unity Fc kwa mambao 5-2.
Maafisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa
PSPF wakiwa kwenye picha ya pamoja na waratibu wa michezo hiyo pamoja
na Timu ya G Unity Fc walioibuka washindi wa wa kwanza baada ya kufunga
timu ya Sukuma Land Fc mabao 5 -2, mchezo huo uliofanyika katika kiwanja
cha Kipunguni B.