Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (kulia), akisalimiana na Afisa Ugavi Mkuu wa Bohari Kuu ya Maji, Datus Bahati mara baada ya kuwasili Bohari Kuu ya Maji wakati wa ziara yake ya siku tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maji katika mkoa wa Dar es Salaam inayosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA) ambapo aliitimisha ziara hiyo Agosti 27, 2015 kwakukagua miradi iliyopo daraja la mpiji na Kerege na maungio ya maji ya wazo.
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Bohari Kuu ya maji iliyoko Boko jijini Dar es Salaam wakati ziara yake ya siku ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maji katika mkoa wa Dar es Salaam inayosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA).
Afisa Ugavi Mkuu wa Bohari Kuu ya Maji, Datus Bahati akisoma taarifa ya utekelezaji wa kazi za Bohari Kuu ya Maji kwa Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (hayupo pichani).
Kushoto ni Meneja Usimamizi Uendeshaji na Mazingira DAWASA, Modesta Mushi, Afisa Ugavi Mkuu wa Bohari Kuu ya Maji, Datus Bahati (kulia) pamoja na Wakandarasi wa miradi hiyo na maofisa kutoka Wizara ya maji na waandishi wa habari wakimskiliza Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla wakati akizungumza (hayupo pichani).