Jul 14, 2015

URAIS TANZANIA; MANABII HAWA WANAKOSEA WAPI?


1098419_219899274830887_151788808_nNabii Josephat Mwingira

WAKATI Tanzania ikiwa katika vuguvugu la kuelekea Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25, 2015, kuliibuka mambo mengi ya kushangaza yaliyoongeza msisimko kwenye mbio za uchaguzi huo na kuonekana kuwa za kipekee zaidi kiasi cha kufuatiliwa kwa ukaribu na watu wengi kuliko chaguzi zilizopita.

komanyaMarehemu Komanya.
Makundi mbalimbali yalibashiri kama siyo kutabiri nani atakuwa rais kwa ujumla. Kwa maana kutoka vyama vingine na ikiwemo Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndicho kinachotawala.
LOWASSA ALITAJWA MARA NYINGI
Taasisi mbalimbali zilifanya utafiti na kuibuka na wagombea wao, lakini jina la waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa lilitajwa mara nyingi na maeneo mengi, zikiwemo taasisi na mitazamo ya watu  mitaani.
NABIIYASPIPAUL1Nabii Bendera
MAKUNDI YA DINI YALIZIDISHA MATUMAINI
Moja kati ya mambo ya kusisimua ni lile la kuibuka kwa baadhi ya manabii au viongozi wa makanisa nchini, wakidai wameoneshwa na Mungu kuwa baadhi ya viongozi waliotangaza nia watakuwa marais kutokana na maono yao.
Manabii hao waliibuka huku kila mmoja  akiwatangazia waumini wake kwamba, mgombea fulani ndiye atakuwa rais 2015, hali iliyowafanya wenye akili wachache wawapuuze baada ya kujiuliza kwamba inawezekanaje Mungu akawatabiria watu tofauti kwa cheo kimoja cha urais?
Wafuatao ni baadhi ya manabii waliowahi kuweka wazi wagombea wao kwa nyakati tofauti kwa maneno ya kuoneshwa kimaono:
Basileus Ezekiel Mabumba
Ni Mchungaji wa Kanisa la Last Glory. Huyu aliwashangaza watu baada ya kuwa kiongozi wa kwanza wa dini kufunguka kuwa, ameoneshwa na Mungu kwamba Edward Lowassa atakuwa rais na kuweka msisitizo kwa kiapo kizito kuwa auawe kama hayo hayatatimia.
Askofu John Komanya
Kwa sasa ni marehemu, apumzike kwa amani. Yeye alikuwa Askofu wa Huduma ya Cathedral of Joy (CoJ) ya Kiluvya jijini Dar. Enzi za uhai wake alisema ameoneshwa na Mungu kuwa, Lowassa atakuwa rais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu 2015.
Nabii Josephat Mwingira
Yeye ni Nabii wa Huduma ya Efatha yenye makao yake makuu, Mwenge, Dar. Aliwahi kusema amepokea maono kutoka kwa Mungu kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu atashinda kinyang’anyiro cha urais na kusisitiza kuwa, hakuna wa kumzuia kwa sababu ukuu umeamriwa juu yake. Lakini Nyalandu naye kama Lowassa alitolewa katika hatua za mwanzoni.
Nabii Yaspi Bendera
Huyu ni Nabii wa Huduma ya The Revelation Church iliyopo Buza Kipera, Dar  ambapo naye aliwahi kutabiri kwamba, Lowassa atashinda kwa kutumia maono yake na utafiti wa Taasisi ya Twaweza uliobainisha kuwa, Lowassa ameongoza ushindi akifuatiwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda huku Dk. Wilbroad Slaa akishika nafasi ya mwisho. Utabiri huo umebuma.
Nabii David Mpanji
Huyu ni Nabii wa Huduma ya Maombezi ya GMCL, Mbeya. Yeye alikuwa tofauti kabisa na wengine ambapo kwa upande wake alimpaka mafuta Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba kuwa atashinda na kuwa rais na kudai amemuona ana roho ya kuongoza.
Hivyo kwa mafuta aliyompaka lazima atakuwa rais huku akimfananisha na Mfalme Daudi wa kwenye Biblia alivyopakwa mafuta na Nabii Samuel na kuwa mfalme wa Israeli.
John Magufuli, kidedea
Pamoja na maono, utafiti na mitazamo, hatimaye, Waziri wa Ujenzi, John Pombe Magufuli ameibuka kidedea kuwa mgombea urais ndani ya chama chake cha CCM akiwaongoza wenzake 38 waliojitokeza kugombea nafasi hiyo.
Juzi, baadhi ya wasomaji wa gazeti hili walizungumza na gazeti hili ambapo hoja yao kubwa ilikuwa ni swali la manabii na wachungaji kutabiri mambo halafu yasitimie, wanakosea wapi?

GPL