Jul 10, 2015

Ni Wakati Wetu Wasanii Kusimama- Steve Nyerere

MWIGIZAJI na mtayarishaji wa filamu Steven Mengele ‘Steve Nyerere’ amefunguka kwa kusema kuwa wasanii wa filamu wana nafasi kubwa katika uongozi kwa ni kivutio cha wapiga kura kwa mantiki ni wakati wao kushiriki katika hatamu za uongozi, na kujiandikisha katika daftari la mpiga kura. "Ni kweli tunahitaji mabadiliko katika utawala lakini hilo litafanikiwa tu pale tutaposhiriki kujiandikisha katika Daftari la mpiga kura, kama nilivyosema badala ya kusimama badala ya mgombea sasa tunasimama sisi tujiandikishe bila kupuuza,”anasema Steve Nyerere.

Msanii huyo mwenye kipaji cha kuigiza kuigiza sauti za viongozi mbalimbali anasema wasanii pamoja na wananchi muda kulalamika umechaguliwa kiongozi husiyemkubali umekwisha lazima kila mtu aache shughuli zake kwa siku moja tu ajiandikishe katika Daftari la mpiga kura kuwapa sapoti.
FC