“Wakati Benjamin Mkapa akiwa madarakani, nilifahamu kwamba atakayefuata ni JK (Jakaya Kikwete), lakini hali ya mwaka huu ni tofauti kwa sababu haujui nani atafuata. Kwa sababu hiyo ipo haja, tena ya makusudi kabisa kuhakikisha umakini wa hali ya juu unachukuliwa katika kila hatua, vinginevyo inaweza kuleta matatizo makubwa,” alisema muigizaji huyo mkongwe akiuzungumzia mchakato huo.
Kamati Kuu (CC-CCM) itaanza kikao chake cha kuchuja majina ya wagombea hao wapatao 37 waliorejesha fomu, ili kupata majina matano yatakayopelekwa mbele ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) inayotarajiwa kukutana kesho, ambayo nayo itawakata wawili kati yao ili watakaobaki waende kupigiwa kura kwenye Mkutano Mkuu utakaofanyika kwa siku mbili za Jumamosi na Jumapili hii.
na GPL