Akizungumza na safu hii katikati ya wiki, Thea alisema kila msanii ana thamani yake kutokana na nafasi yake katika kazi ya Filamu . Hivyo ametaka wathaminiwe kulingana na kazi zao badala ya kuwawekea vizuizi vinavyokwamisha maendeleo ya vipaji vyao .
"MIMI nimeshirikishwa katika Filamu na wasanii ambao hawana nafasi na nimeona kazi zao ni nzuri kuliko hata hao wasanii ambao wanajulikana hapa nchini", alisema Thea.
