Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Fedha,
Ingiahedi Mduma akifafanua jambo wakati wa warsha ya siku tano kuhusu
mradi wa maboresho ya matumizi ya fedha za umma inayoendelea katika
Hoteli Njuweni Kibaha. Bi.Ingiahedi alisema kuwa Serikali
ya Tanzania ilianzisha mradi huo kwa madhumuni ya kuimarisha mifumo ya
matumizi ya fedha katika ngazi zote. Mradi huu umekuwa wa awamu 4
kutokana na mafanikio yanayojitokeza na changamoto.
Alisema kuwa Mpaka
sasa mradi huo umepata mafanikio makubwa hasa ya kuweka mfumo mzuri wa
malipo, muda wa kupitishwa kwa bajeti ya Taifa umeimarika na fedha
zinatoka kwa wakati,Alibainisha kuwa bajeti ya mwananchi inatangazwa
katika Tovuti ya Wizara ya fedha na kuwa mfumo wa malipo umefika mpaka
katika Serikali za Mitaa.
Washiriki wa warsha kuhusu maboresho ya matumizi ya fedha za umma inayoendelea katika Hoteli ya Njuweni Kibaha.
Baadhi
ya waandishi wa Habari wakiwa katika warsha ya siku tano kuhusu kuhusu
mradi wa maboresho ya matumizi ya fedha za umma inayoendelea katika
Hoteli ya Njuweni Kibaha.
=========== ======= ========
Serikali
ya Tanzania ilianzisha mradi huo kwa madhumuni ya kuimarisha mifumo ya
matumizi ya fedha katika ngazi zote. Mradi huu umekuwa wa awamu 4
kutokana na mafanikio yanayojitokeza na changamoto.
Awamu ya kwanza (I) ilikuwa kutoka mwaka
1998 – 2004 huu ulikuwa na malengo ya kudhibiti matumizi,
kuweka nidhamu ya fedha pamoja na kukuzana kuimarisha uchumi mpana.
1998 – 2004 huu ulikuwa na malengo ya kudhibiti matumizi,
kuweka nidhamu ya fedha pamoja na kukuzana kuimarisha uchumi mpana.
Awamu ya pili (II)
ilikuwa kutoka mwaka 2004 – 2008 malengo ya mradi huo yalikuwa ni kuimarisha na kuendeleza mifumo na njia zinazotumika katika malipo ya fedha za umma kwa kutumia njia rahisi na nyepesi. Aidha awamu hiyo ilizingatia pia uimarishaji wa njia ya ukusanyaji mapato na jinsi ya kuweka mbinu ya kuzitumia rasilimali fedha na kuweka mikakati ya kipi kianze kwanza.
ilikuwa kutoka mwaka 2004 – 2008 malengo ya mradi huo yalikuwa ni kuimarisha na kuendeleza mifumo na njia zinazotumika katika malipo ya fedha za umma kwa kutumia njia rahisi na nyepesi. Aidha awamu hiyo ilizingatia pia uimarishaji wa njia ya ukusanyaji mapato na jinsi ya kuweka mbinu ya kuzitumia rasilimali fedha na kuweka mikakati ya kipi kianze kwanza.
Awamu ya tatu (III)
ilikua kuanzia 2008 – 2011, mradi huu ulikua na malengo ya kuhakikisha kuna kuwa na upatikanaji rasilimali fedha kutoka katikaTaasisi mbalimbali za kifedha.
ilikua kuanzia 2008 – 2011, mradi huu ulikua na malengo ya kuhakikisha kuna kuwa na upatikanaji rasilimali fedha kutoka katikaTaasisi mbalimbali za kifedha.
Awamu ya nne (IV)
ya mradi ni kuanzia June 2012, mradi ulizinduliwa na kuanza rasmi tarehe 1 Julai, 2012. Madhumuni ya mradi huu katika awamu ya nne umelenga katika kuonge za nguvu ambayo itawezesha kufikia malengo ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025, hiyo inaenda sanjari na mpango wa maendeleo wa miaka mitano yaani 2011/2012 – 2015/2016 na MKUKUTA (MkakatiwaKukuzauchumi Tanzania)/ MKUZA (Mkakati wa Kukuza uchumi Zanzibar), ili kufika malengo ya ukuaji wa uchumi.
HABARI ZAIDI INGIA HAPA
ya mradi ni kuanzia June 2012, mradi ulizinduliwa na kuanza rasmi tarehe 1 Julai, 2012. Madhumuni ya mradi huu katika awamu ya nne umelenga katika kuonge za nguvu ambayo itawezesha kufikia malengo ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025, hiyo inaenda sanjari na mpango wa maendeleo wa miaka mitano yaani 2011/2012 – 2015/2016 na MKUKUTA (MkakatiwaKukuzauchumi Tanzania)/ MKUZA (Mkakati wa Kukuza uchumi Zanzibar), ili kufika malengo ya ukuaji wa uchumi.
HABARI ZAIDI INGIA HAPA