
Wanachama hao sita ni;-
i. January Makamba
ii. William Ngeleja
iii. Steven Wassira
iv. Bernard Membe
v. Edward Lowassa
vi. Fredrick Sumaye
Kamati
Kuu imepokea na kukubali pendekezo la Kamati ya Usalama na Maadili ya
kumalizaka kwa kipindi cha adhabu kwa wanachama hawa. Kwa hiyo adhabu
hiyo kwa sasa imemalizika, na wanachama hao wameruhusiwa kuendelea na
shughuli zao katika Chama.
Hata
hivyo Kamati Kuu inawataka wanachama hawa na wale wengine wenye nia ya
kugombea Urais kupitia CCM Kuzisoma , Kuziheshimu na Kuzizingatia Kanuni
za Maadili za CCM na kanuni zingine zinazoongoza mchakato ndani ya
Chama, ili wasikumbwe na adhabu itokanayo na kuzivunja kanuni hizo.
Wale
wote wanaotaka kugombea, yaani waliokuwa kwenye adhabu na wengine
watakaojiingiza kwenye kampeni mapema na hivyo kukiuka maadili na miiko
ya Chama, taarifa za kukiuka kwao zitatumiwa wakati wa kuchuja majina ya
wagombea utakapofika.
Taarifa
hizo zitatumika katika kuwapima na kuamua iwapo wana sifa za kutosha na
wanafaa au hawafai katika kupata uteuzi wa nafasi wanayoiomba.
Imetolewa na;-
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM
22/05/2015