May 20, 2015

MOCHRISPO SECURITY YAZIDI KUBORESHA ASKARI WAKE

Askari wa MOCHRISPO SECURITY baada ya parade wakipata picha ya pamoja
askari wakakamavu wa Mochrispo security co.ltd wakijiandaa kwa kuingia mzigoni baada ya mazoezi makali ya asubuhi tayari wakiwa wameishapangiwa majukumu ya kazi zao
picha na Mkurugenzi wa Mochrispo security

Mochrispo security inatoa nafasi za mafunzo kwa askari wake wanaofanya vizuri zaidi kazini na kuwajengea uwezo wa kujiajiri na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi ndani na nje ya Tanzania. takaribani askari 16 tayari wameishapata mafunzo ya kozi za awali za computer na tayari wapo katika vitengo maalumu vya kiusalama ndani ya kampuni hiyo.

Kampuni ya MOCHRISPO SECURITY iliyopo jijini Mwanza imekuwa ikifanya vyema kazi zake katika kuboresha na kuimarisha mazingira ya ulinzi na usalama wa raia na mali zao. kampuni hii inawafanyakazi wengi wapatao 200 ndani ya na nje ya jiji la mwanza. imekuwa ikitoa fursa pekee kwa wafanyakazi na askari wake wote wanaofanya vyema katika mazingira yao ya kazi kwani wanapewa vipaumbele. kwa kupewa ofa za kozi mbalimbali za computer na mafunzo ya ufundi katika fani hizo. Mkurugenzi wa kampuni ya MOCHRISPO anatoa pongezi kwa wafanyakazi wake wote na kuwataka wawe makini katika kazi zao na watimize majukumu yao kama wanavyopangiwa

KWA MAHITAJI YA ULINZI WASILIANA NA 
MOCHRISPO SECURITY CO.LTD
+255 752 203 33 33
+255 783777880
EMAIL: mochrispo@gmail.com