Mwenyekiti
wa Misa-Tanzania-Media Institute of Southern Africa (Taasisi ya vyombo
vya habari Kusini mwa Afrika) Bwana Simon Berege akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na maadhimisho ya siku ya
uhuru wa habari duniani (WPFD) yatakayofanyika tarehe 2 mwezi Mei mwaka
huu mkoani Morogoro.
Mkurugenzi
wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) ambao ni miongoni mwa
wadau wa maandalizi ya maadhimisho hayo Bw. Ernest Sungura akifafanua
jambo katika mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) uliofanyika
katika hoteli ya Holiday Inn jijini Dar es Salaam leo. Kulia Mwakilishi
wa Umoja wa Mataifa ambao ni miongoni mwa wadhamini wa maadhimisho
hayo, Usia Nkhoma Ledama.
Makamu
Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waancdishi wa habari nchini (UTPC), Jane
Mihanji akisisitiza umuhimu wa wanahabari kuhudhuria maadhimisho ya siku
ya uhuru wa habari duniani (WPFD) ambayo kitaifa yanatarajiwa kufanyika
mkoani Morogoro Mei 2 mwaka huu. Katikati ni Mwakilishi wa Umoja wa
Mataifa ambao ni miongoni mwa wadhamini wa maadhimisho hayo, Usia Nkhoma
Ledama na kushoto ni Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania
(TMF) ambao ni miongoni mwa wadau wa maandalizi ya maadhimisho hayo Bw.
Ernest Sungura.
Miongoni
mwa wadau wa maandalizi ya maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari
duniani (WPFD) Bw.Richard Shaba kutoka KAS Tanzania na Mwakilishi kutoka
TAMWA, Godrida Jola wakisikiliza maswali kutoka kwa wanahabari (hawapo
pichani).