Mar 23, 2015

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AANZA ZIARA MKOA WA KILIMANJARO

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikatisha kwenye migomba alipokuwa akikagua mifereji ya inayotiririsha maji kuelekea kwenye mashamba ya ndizi akiongozana na Mh. Agrey Mwanri.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka kwenye chumba cha maabara cha hospitali ya wilaya Siha mara baada ya kuyakagua magari matatu ya kubebea wagonjwa.
Sehemu ya jengo la hospitali hiyo ya wilaya ya Siha kama lionekanavyo pichani,ambapo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alikwenda kukagua.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya bwawa la umwagiliaji la Kishisha kata ya Ivaeny  kutoka kwa mbunge wa jimbo hilo Mh. Agrey Mwanri wakati alipokagua bwawa hilo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akichukua ndizi wakati alipowatembelea akina mama wajasiriamali kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa CCM wa wilaya ya Siha.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa akina mama wajasiamali  wakimasai wanaojishughulisha na kutengeneza bidhaa za urembo kwenye mkutano wa hadhara uwanja wa CCM Siha.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuzindua ofisi ya CCM wilaya ya Siha, kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo Ndugu Oscar Temu.
 Ndugu Kinana akitoka nje ya ofisi hiyo mara baada ya kuweka jiwe la msingi na kuikagua.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti wa kumbukumbu nje ya ofisi ya wilaya ya CCM Siha.
Mbunge wa jimbo la Siha Mh. Agrey Mwanri akimpongeza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya hotuba yake katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivalishwa skafu kutoka  kwa vijana wa Chipukizi wakati alipowasili katika shule ya sekondari ya Nuru wilaya ya Siha, Kutoka kulia ni Mbunge wa jimbo la Siha Mh. Agrey Mwanri na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Leonidas Gama akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipowasili mapema leo wilaya ya siha.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  na viongozi wengine wa CCM wakishiriki kazi ya kumimina zege kwenye shule ya sekondari ya Nuru.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati akikagua daraja la Embokoi na Mungushi ambalo limejengwa ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM wilayani Siha.
 Baadhi ya wananchi waliofurika katika mkutano huo.
 Mbunge wa jimbo la Siha Mh. Agrey Mwanri akiwahutubia wananchi katika mkutano huo.
 Baadhi ya wananchi akijizuia mvua na viti wakati mkutano huo ulipokuwa ukiendelea.
 Wananchi waliendelea kunyeshewa na mvua ili kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati akiwahutubia.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi huku mvua ikinyesha hata hivyo wananchi hao waliamua kujikinga na viti walivyokuwa wamevikalia ili wamsikilize Ndugu Kinana.
 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana amewasili katika jimbo la Siha, katika ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua kuhimiza na kusimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ambayo katika jimbo la Siha imetekelezwa kwa asilimia kubwa ikisimamiwa na Mbunge wa jimbo hilo na Naibu Waziri wa TAMISEMI Mh. Agrey Mwanri.
Akielezea utekelezaji wa ilani ya uchaguzi katika jimbo hilo Mh. Agrey Mwanri amesema ilani ya CCM imetekelezwa kwa kiwango kikubwa ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo vina maji safi na salama ya kunywa, Umeme umefika katika vijiji vyote kinachondelelea ni usambazaji kwa kila mwananchi, Suala la huduma za afya nalo liko vizuri kwani vimejenga vituo vya afya karibu kila maeneo na baadhi ya zahanati zinamaliziwa kujengwa.
Suala la Elimu wakati mbunge huyo akiinga madarakani Siha kulikuwa na sekondari moja, lakini sasa kuna sekondari 17 na ufaulu wa wanafunzi umeongezeka kwa kiwangi cha juu, Maabara zinakamilishwa ambapo mabati yamesambazwa karibu kila shule ili kukamilisha ujenzi wa maabara hizo.
Akizungumza katika mkutano huo pamoja na mambo mengine Katibu Mkuu wa CCM amemsifu Mh. Agrey Mwanri kwa kazi aliyoifanya katika jimbo hilo kwa kufanya kazi vizuri na kuwaletea wananchi maendeleo na kuwaambia wananchi katika mkutano huo kwamba kama kiongozi anafanya kazi nzuri hakuna haja ya kubadilisha viongozi kama mashati, Mwacheni awaleteeni maendeleo.
Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape nnauye Katubu wa NEC Itikadi na Uenezi.