Jan 15, 2015

Riyama: Nimempita Baba Watoto Wangu Miaka 10

Mwigizaji Riyama Ally amefunguka kwa kinywa chake kuwa baba aliyezaa naye mtoto wake wa kike aitwaye Fatma, amempita takriban miaka 10.Riyama alizungumza hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi kimoja cha TV na kusema kuwa hakuna chochote kinachohusiana na umri katika suala la mapenzi kwa sababu ingekuwa kuna tatizo basi kwa upande wake ingekuwa shida.
“ Jamani sidhani kama kuna uhusiano wowote wa umri katika mapenzi, mimi nimempita baba mtoto wangu miaka 10 na hata mpenzi wangu wa sasa naye nimempita hivyohivyo, umri hauna nafasi kabisa kwangu,” alisema Riyama.
PICHA:Riyama Ally akiwa na baba watoto wake.