Mama wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa ambaye kwasasa
ameingia kwenye tasnia ya filamu hapa nchini amefunguka kuwa hakuna
skendo ambayo ilimsononesha kama ile ya mwanaye huyo kuambiwa hajui
Kiingereza .
Mama Kanumba alifunguka hayo juzikati katika mahojiano maalum na
Mwandishi Wetu : “Eti Kanumba hajui Kiingereza , hili lilinishtua sana
nikalipinga kwa nguvu zote sababu najua mwanangu hata shule alikuwa
kichwa, ” alisema mama Kanumba .
Skendo ya kudaiwa kutozungumza Kiingereza kibovu iliibuka mwaka 2009
katika Jumba la Big Brother Afrika Kusini wakati Kanumba alipoalikwa
kutembelea mjengo huo.
Mama kanumba ameshaingia kwenye sanaa ya uigizaji na ameshafanya kazi
nzuri kwenye filamu iitwayo MAPENZI YA MUNGU ambayo ameigiza na mastaa
kadhaa akiwemo Elizabeth Michael aka Lulu na mwanamziki Linnah Sanga.
Bongo movie.com
