Nov 2, 2014

VURUGU: NGUMI ZAPIGWA WAKATI WA MDAHALO WA KATIBA



Jaji Warioba.
VURUGU zilizoambatana na ngumi kurushwa zimetokea hivi punde katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam wakati aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba alipokuwa akitoa mada kwenye mdahalo wa kujadili umuhimu wa kuielewa kwa kina Katiba inayopendekezwa kama ilivyopitishwa na Bunge Maalum la Katiba.
Vurugu hizo zimezuka baada ya watu waliokuwa na mabango kuvamia ukumbuni hapo na kusababisha baadhi ya watu waliokuwa wanafuatilia mdahalo huo kuwakabili na kuwapa kichapo.
Baada ya vurugu hizo, mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere na kurushwa moja kwa moja na ITV umesimamishwa kwa muda.


Mdahalo mkubwa ulioandaliwa na taasisi ya Mwalimu Nyerere wakatishwa ghafla baada ya kuibuka ugomvi mkubwa. Watu wasiofahamika walisimama na Mabango yaliokuwa yanaonyesha kukubaliana na katiba inayopendekezwa wakati mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya katiba Waziri mkuu mstafu Jaji Warioba alipokuwa anahitimisha hotuba yake kama mchangiaji wa kwanza. 

Je ni Kweli CCM wameandaa watu kwenda kumzomea Warioba ?