Jun 13, 2014

VURUGU ZA WAMACHINGA MWANZA MABOMU YA MACHOZI YARINDIMA ZAIDI YA SAA 3, BIASHARA ZAFUNGWA KABISA.

 Hakuna biashara kila mtaa uligeuka kuwa mchungu.

 hapakaliki hapa 

Eneo hili la kutoka barabara ya Lumumba linaloingia Makoroboi hadi kupitia msikiti wa Hindu (ukuta wa mahala panapo zimwa moto) na kuingia barabara ya Nyerere linatakiwa kuwa wazi bila kuwa na wafanyabiashara wanaotandaza bidhaa zao chini au kuegesha kunye kuta, na tukio la leo ni la zaidi ya mara mbili kutokea kwa wamachinga  kulikalia kwa nguvu.



 Oparesheni ofisa wa zima moto, Sajenti meja Gadafi Masoud  amesema msikiti wa Hindu wanaosali masinga singa umenusurika kuchomwa moto na machinga hao baada ya magari makubwa mawili kikosi chake kuuzima moto uliowashwa na wamachinga kwa lengo la kuuteketeza msikiti huo ulio katika eneo waliloondolewa

 mtaa kwa mtaa hapatoshi 

 hakuna cha gari wala mtu hata ndege wa anagani walitoweka kabisa


 tunawafata huko huko


 Vijana waandamanaji wakifunga barabara, ingawa kuna walakini je hawa nao ni machinga? Abdukadri Salim anasema kuwa vijana wanatumiwa kufanya vurugu na siyowamachinga

 Jeshi la polisi katika doria mtaa kwa mtaa.


 Jeshi la wananchi lilitoa askari wake wa kijeshi “MP” kuimarisha ulinzi kwenye vitengo vya mabenki, ofisi za serikali na maeneo nyeti ili kutokwaza shughuli za kila siku kuendelea.

 Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Valentino Mlowola hakuweza kupatikana kwa kuwa yuko safari kikazi na msaidizi wake Christopher Fuime alidaiwa kuwa katika oparesheni hiyo huku baadhi ya askari ambao hawakutaka  kutajwa majina yao wakisema zaidi ya wamachinga 40 wamekamatwa  kuhusiana na vurugu hizo.

 KATIKATI ya jiji la Mwanza leo paligeuka kuwa pachungu baada ya mabomu zaidi ya 120 kulindima toka saa 3:58 asubuhi hadi 8:45 na kulifanya eneo hilo lisikalike.
Mabomu hayo yalilindima maeneo mbalimbali ya mji ikiwemo eneo  maarufu la Makoroboi  kufuatia kuvunjwa kwa vibanda vya machinga jana asubuhi hali iliyowafanya wacharuke na kuanza mapambano na askari polisi na mgambo wa Jiji huku wakishinikiza wenzao walio kwenye maeneo halali nao waondolewe ili wote waikose makoroboi.

Katika sekeseke hilo wamachinga  zaidi ya 40 wamekamatwa kwa kukiuka sheria za mipango miji.