Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Jacob Zuma wakiwa wamesimama huku Nyimbo za Mataifa mawili zikiimbwa Ikulu jijini Dar es salaam Mei 11, 2017.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema amemuomba Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Jacob Zuma amuombee mkopo katika Umoja wa nchi tajiri BRICS ambapo Afrika Kusini nao wapo katika umoja huo.
Rais
Magufuli amesema hayo leo Ikulu wakati wakisaini mikataba ya
ushirikiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini ambapo wamekubaliana
kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwepo ushirikiano wa kiuchumi,
utalii, na sekta ya sayansi na teknolojia.
"Nimemshukuru Rais Jacob
Zuma kwa ujumbe wake na kuongozana na wafanyabiashara kutoka Afrika ya
Kusini, ambao saizi wanakutana na wafanyabiashara wa kwetu jambo ambalo
litaweza kuongeza uhusino wa kibiashara, tumekubaliana kuendelea
kushirikiana ili kukuza fursa kati yetu, tumekubaliana nchi zetu kuondoa
vikwazo vya kiuchumi ili tuweze kupiga hatua zaidi. Lakini pia
nimemuomba Rais Zuma kutusaidia kupata mkopo wa bei nafuu katika umoja
wao wa (BRICS) nchi tajiri ili usaidie ujenzi wa Reli ya standard gauge
na amenihakikishia atafanya hivyo" alisema Rais Magufuli
Mbali na hilo Rais Magufuli alimuomba Rais Zuma kuja kuchukua walimu
wa Kiswahili nchini ili wakafundishe Kiswahili huko Afrika Kusini na
kuzisi kuimarisha umoja wao, kwa upande wake Rais Jacob Zuma alishukuru
mwaliko wa Rais Magufuli na kusema amefurahia sana huku akiahidi
kuendeleza umoja na undugu huo kwa kutekeleza yale ambayo wamekubaliana.