
Taarifa
iliyoifikia asubuhi hii, inaeleza kuwa Bondia maarufu
nchini, Thomas Mashali amekutwa amefariki dunia usiku wa kuamkia leo na
mwili wake kukutwa maeneo ya Tabata, Jijini Dar es salaam. akithibitisha
kutokea kwa kifo cha mwanamasumbwi huyo, Bondia Abdallah Pazi (Dullah
Mbabe) amesema Mashali amefikwa na umauti huo usiku wa kumkia leo kwa
kudaiwa kupigwa mpaka kuuawa na watu wasiojulikana kwa tuhuma za wizi.
tutaendelea kujuzana taarifa zaidi za msiba huu wa Mwanamasumbwi huyu
nguli hapa nchini, endelea kutembelea Libeneke la Globu ya Jamii.